Kwa mujibu wa gazeti la Al-Raya, Waislamu hao wanajumuisha wanaume 141 na wanawake 42 kutoka nchi mbali mbali duniani na watashindano katika kuhifadhi na kusoma (tarteel) sura fupi fupi za Qur’ani Tukufu.
Kamati andalizi ya mashindano ya kitaifa ya Qur’ani imetangaza kuwa, ililinganishwa na mashindano ya miaka miwili iliyopita, mwaka huu kuna washiriki 77 zaidi.
Lengo la mashindano hayo limetajwa kuwa ni kuwahimiza na kuwawezesha waliosilimu kujifunza misingi ya Qur’ani Tukufu.
Aidha mashindano hayo ya Qur’ani yanalenga kueneza thamani za Qur’ani na Kiislamu miongoni mwa waliosilimu ili waweze kutekeleza Uislamu katika maisha yao.../mh