Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, vituo hivyo maalumu kwa wanawake vimewekwa katika njia zote za kuelekea Karbala ambapo wafanyaziara watapata fursa ya kutulia na kutafakari kuhusu aya za Qur'ani Tukufu.
Mmoja wa wahusika wa mpango huo, Fatima Ismail amesema Ziara ya Siku ya Arubaini ni fursa kwa ajili ya kustawisah utamaduni wa kutafakri kuhusu aya za Qur'ani.
Amesema wanawake wanaosimama katika vituo hivyo kutafakari kuhusu Qur'ani baadaye watakuwa mabalozi wa kueneza utamaduni wa Qur'ani katika jamii zao.
Wanoshukia katika vituo hivyo wanasoma aya kadhaa a Qur'ani, kanunu za tajwidi na kusha kujadili masuala ya kifiqhi n.k
Inafaa kukumbusha hapa kuwa, majlisi na ziara ya siku ya Arubaini
hufanyika kila mwaka tarehe 20 Safar, kwa mujibu wa kalenda ya Hijria
Qamaria, baada ya kupita siku Arubaini tangu tarehe 10 mwezi wa
Muharram kwa ajili ya kukumbuka kuuawa shahidi mjukuu wa Mtume SAW, Imam
Hussein AS
na masahaba zake ambao walijitolea roho zao kwa ajili ya kuhuisha dini
ya
Mwenyezi Mungu katika jangwa la Karbala.