Uundaji wa apu hiyo umefadhiliwa na Wakfu wa Abdullah al-Raji. Aou hiyo Inachanganya michezo na mbinu za kufundishia kwa elimu ya Qur'ani.
Programu hiyo huwasaidia watoto kujifunza kusoma Qur’ani Tukufu kwa namna ya visa vya kuelimisha ambapo watoto hufuatana na Salim, mvulana mwenye akili na busara akiwa na ndege wake, katika safari.
Wanapitia hatua mbalimbali, ambazo huwa ngumu kupita kadri safari inavyoendelea, ili kurudisha masanduku ya nuru yaliyoibiwa na viumbe wa kishetani.
Safari inapoendelea, watoto, kupitia michezo ya kufurahisha na kuburudisha, hujifunza jinsi ya kutamka kwa usahihi maneno ya Sura za Qur’ani Tukufu.
Teknolojia na programu mbalimbali mpya, ikiwa ni pamoja na zana za utambuzi wa usemi zinazoendeshwa na Akili Mnemba au Artificial Intellligence AI, zimetumika kutengeneza apu hii
Abdul Rahman bin Khazir al-Khazir, afisa wa Jumuiya ya Kuhudumia Quran na Sunnah ya Al-Burhan, alisema wazo la kuunda apu ya aina hiyo liliibuliwa baada ya jamii kutambua hitaji la familia za Kiislamu kuwa na programu inayofundisha Quran kwa watoto kwa njia rahisi.
4188553