IQNA

Qiraa ya Mahmoud Shahat Anwar katika Ufunguzi wa Mashindano ya Qur'ani ya Port Said 2024

19:12 - February 05, 2024
Habari ID: 3478308
IQNA - Qari mashuhuri wa Misri Mahmoud Shahat Anwar alikariri aya za 107-110 za Surah Al-Kahf katika sherehe za uzinduzi wa toleo la 7 Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Port Said.
Hafla hiyo ilifanyika mnamo Februari 2, 2024, huko Port Said na viongozi wa nchi na washiriki kutoka nchi 50 walihudhuria.
Mashindano hayo yameandaliwa katika kategoria za kuhifadhi Qur'ani Tukufu na Ibtihal. Toleo la mwaka huu limepewa jina la qari maarufu wa Misri Sheikh Shahat Muhammad Anwar (1950-2008), marehemu babake Mahmoud Shahat Anwar.
captcha