IQNA

Hizbullah yatoa taarifa baada ya kuvurumisha maroketi katika kambi za kijeshi za Israel

20:12 - August 06, 2021
Habari ID: 3474165
TEHRAN (IQNA)- Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetoa taarifa na kusema wapiganaji wake wa kituo cha Shahidi Ali Muhsin Kamel na Shahidi Muhammad Qassim Tahal wamejibu mashambulizi ya karibuni ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ardhi ya Lebanon kwa kuvurumisha maroketi kadhaa dhidi ya vituo vya kijeshi vya utawala huo.

Taarifa iliyotolewa na Hizbullah imesema kuwa, mapema leo, kambi za jeshi la utawala wa Kizayuni Israel katika eneo la Lebanon linalokaliwa kwa mabavu na utawala huo la Mashamba ya Shebaa zimeshambuliwa kwa makumi ya maroketi ya wapiganaji wa harakati hiyo. 

Taatifa hiyo ya Hizbullah imeongeza kuwa, mashambulizi hayo ni jibu kwa mashambulizi ya anga yaliyofanywa jana na utawala wa Kizayuni dhidi ya maeneo kadhaa ya miiniko ya Kafr Shuba. 

Kufuatia mashambulizi hayo ya kulipiza kisasi, Waziri Mkuu wa Israeli Naftali Bennett na Waziri wa Vita, Benny Gantz walifanya kikao cha dharura kujadili suala hilo

Televisheni ya Al Mayadeen ya Lebanon imesema maroketi yasiyopungua 20 yalirushwa dhidi ya vituo vya jeshi la Israeli. Televisheni ya Al-Minar pia imesema maroketi kadhaa yalilenga kituo cha jeshi la Israel cha Douf.

Aoun pia amesema mashambulizi hayo ya Israel ni tishio la moja kwa moja kwa usalama na amani ya kusini mwa Lebanon na yamekiuka maazimio ya Baraza la Usalama la UN.

 

3988750

captcha